Jinsi ya kupika Mchuzi Wa Nyama Ya Kusaga Na Mayai

 


Vipimo


Nyama ya kusaga - 2 LB (Ratili)


Mayai -  6


Vitunguu -  4


Kitunguu saumu(thomu/galic) na Tangawizi - 1 Kijiko cha supu


Pilipili mbichi iliyosagwa - 1 Kijiko cha chai


Nyanya iliyokatwa katwa - 4


Kotmiri - ½ Kikombe


Pilipili Manga - ¼Kijiko cha chai


Bizari ya curry -  ½ Kijiko cha chai


Nyanya ya kopo -  3 Vijiko vya supu


Garam masala - 1 Kijiko cha supu


Mafuta ya kukaangia - Kiasi


Namna Ya Kutayarisha Na Kupika  


Chemsha mayai, yakiiva ambua maganda na uweke kando.

Katika sufuria weka mafuta yapate moto, Kaanga vitunguu hadi vigeuke na kuwa rangi ya hudhurungi.

Halafu tia thomu na tangawizi kanga kidogo tu, kisha tia bizari zote na pilipili uendelee kukaanga.

Kisha weka nyama na uiache motoni huku unakoroga hadi iwe si nyekundu tena.

Tia nyanya na chumvi ziache zilainike halafu tia nyanya ya kopo.

Ongeza maji kiasi unavyopenda mchuzi wako kuwa mzito au mwepesi.

Kisha weka yale mayai ya kuchemsha na iache itokote kidogo kwa moto mdogo.

Mwishoe mwagia kotmiri, changanya na umimine katika bakuli na itakuwa tayari kwa kuliwa na wali au mkate upendayo.

0 Comments

banner

Ahsante kwa kutembelea zotekali blog ili kuwa karibu nasi kila wakati Jiunge katika kurasa zetu zamitandao ya kijamii  facebook , Twitter, Instagram na Youtube  NI BUREE