Wakimbilia kwa waganga wa kienyeji kutibu Kifua Kikuu

 Kukosekana kwa elimu ya Wataalam wa afya waliobobea katika kuwahudumia wagonjwa kila siku, imewafanya baadhi ya Wananchi kwenda kwa waganga wa kienyeji kupata tiba za ugonjwa wa Kifua Kikuu wakidhani kuwa wamerogwa.


Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Hospitali Maalumu ya Taifa ya Magonjwa Ambukizi Kibong’oto Dkt. Leonard Subi wakati akizungumza kwenye ufunguzi wa zoezi la upimaji wa ugonjwa wa Kifua Kikuu, Virusi vya Ukimwi, shinikizo la damu, zoezi lililofanyika katika kitongoji cha Orengetwa Kata ya Sanya Juu Wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro.


Dkt. Subi amesema kukosekana kwa elimu hiyo, imesababisha baadhi ya Wananchi kukimbilia kwa waganga wa kienyeji wakidhani wamerogwa kabla hawajagundua kama wanaumwa Kifua Kikuu.


Dkt. Subi amesema takwimu zinaonyesha kuwa watu zaidi ya milioni 10.4 wanaugua Kifua Kikuu kila mwaka na kati yao watu milioni 1.6 wanafariki dunia kutokana na ugonjwa wa Kifua Kikuu (TB) na nchi ya Tanzania inatajwa kuwa ni miongoni mwa nchi duniani yenye maambukizi ya Kifua Kikuu ambayo yako juu.

0 Comments

banner

Ahsante kwa kutembelea zotekali blog ili kuwa karibu nasi kila wakati Jiunge katika kurasa zetu zamitandao ya kijamii  facebook , Twitter, Instagram na Youtube  NI BUREE