Bwanyenye Wa Amerika Akashifu Serikali Ya Ruto Kwa Kutenga Jumatatu Kuwa Sikukuu Ya Upanzi Miti

 MTAALAMU wa Teknolojia ya Fedha (Fintech) ambaye ni mwajiri nchini Kenya, Jason Marshall, amekashifu serikali kwa kutangaza Jumatatu, Novemba 13, 2023 kuwa Sikukuu.



Serikali ilishangaza Wakenya kwa kutangaza kuwa leo, Jumatatu itakuwa Sikukuu kwa minajili ya upanzi wa miti nchini.


“Siku hii, wananchi wote wanatarajiwa kupanda miti kuonyesha uzalendo kwa juhudi za kitaifa za kuokoa nchi dhidi ya athari mbaya ya mabadiliko ya tabianchi,” alitangaza Waziri wa Usalama wa Ndani, Prof Kithure Kindiki kupitia Gazeti Rasmi la Serikali Novemba 6, 2023.


Tangazo hili lilimkera Bw Jason Marshall, ambaye ni mwajiri kutoka Amerika akishangaa ni kwa nini wafanyakazi wake washerehekee upandaji miti, badala ya kufanya kazi.

ka katika akaunti yake ya mtandao wa kijamii wa X (awali Twitter).


Mwajiri huyu amelinganisha taifa la Kenya na America (US), akisema nchi yake ina Sikukuu chache.


Kulingana na Bw Marshall, Kenya husherehekea Sikukuu ambazo hazina maana.

“Kule Amerika, Sikukuu ni za serikali na wafanyakazi wa benki tu,” alisema.


“Wanabenki na wafanyakazi wa serikali huwa na Sikukuu 11. Wafanyakazi wa sekta ya kibinafsi huwa na siku ya mapumziko 7 ama 8 Amerika,” aliongeza.


Kulingana na bwanyenye Marshall, kampuni yake itagharamika kulipa wafanyakazi wake licha ya wao kuadhimisha Sikukuu ambayo anasema walipewa bure.

Siku hii, serikali inalenga kupanda miche 100 milioni kote nchini.


Wakenya wanaoshiriki upandaji miti wanatakiwa kupokea miche kutoka kwa afisi za chifu zilizo karibu nao bila malipo.


Mwaka uliopita, 2022, Rais William Ruto alizindua kampeni ya upanzi wa miti bilioni 15 kufikia 2032.

0 Comments

banner

Ahsante kwa kutembelea zotekali blog ili kuwa karibu nasi kila wakati Jiunge katika kurasa zetu zamitandao ya kijamii  facebook , Twitter, Instagram na Youtube  NI BUREE