Mgambo kupewa kipaumbele ulinzi wa taifa

 MKUU wa Wilaya ya Same, Kasilda Mgeni ameutaka uongozi wa halmashauri hiyo na viongozi wengine wa taasisi za umma na binafsi kutoa kipaumbele kwa vijana waliofuzu mafunzo ya Jeshi la Akiba(Mgambo) kuimarisha ulinzi na shughuli nyingine za ujenzi wa taifa.



DC Mgeni amesema hayo jana wakati akihitimisha mafunzo kwa askari 106 wilayani humo akiwataka askari hao kuzingatia kiapo na kuwa mstari wa mbele kupambana na maovu.


“Niwahakikishie vijana wetu serikali itaweka kipaumbele kuhakikisha inapotokea fursa yoyote mnapewa kipaumbele iwe shughuli zilizo chini ya Halmashauri ikiwemo ulinzi, kusimamia makusanyo ya mapato, kukimbiza mwenge na nafasi za JKT mnachopaswa kuzingatia ni uadilifu na kuviishi viapo mlivyo apa baada ya kuhitimu mafunzo”.Alisema mkuu huyo wa wilaya.


Amewataka pia wahitimu hao kuangalia uwezekano wa kuwaendeleza kielimu kwa kusoma kozi mbalimbali ikiwemo udereva, ufundi umeme na uwashi ili kujijengezea ujuzi na sifa za kuwa na vyeti ambavyo vitawasaidia.

0 Comments

banner

Ahsante kwa kutembelea zotekali blog ili kuwa karibu nasi kila wakati Jiunge katika kurasa zetu zamitandao ya kijamii  facebook , Twitter, Instagram na Youtube  NI BUREE