Kwanini Huna Consistency⁉️


Kwanini Huna Consistency
⁉️ Tatizo ni kubwa kuliko unavyodhani. Wengi wanaanza biashara na kuishia njiani. Wengi wanakata tamaa kwenye mishe zao na kuanza mpya. Haya Mambo 5 yatakayokusaidia kuwa na Nidhamu na Consistency ya hali ya juu. Madini Time... Repost Wengi Wajifunze. 1. Kusudi la maisha ni nuru. Hakuna kitu kizuri kama kila siku unakuwa uanfanya mambo yanayosogeza ndoto zako mbele. Watu wengi wanaishi bila kujua wanataka nini kwenye maisha. Kila siku ni wakati wa kusukuma ndoto yako. Usipokuwa na kusudi utapotea... Kutokuwa na kusudi ni sawa na rubani anayenyanyua ndege akiwa hajui anaenda wapi. Sasa usipokuwa na kusudi utakuwa consistent kwenye nini? You see! 2. Malengo yatakusaidia kupata ramani ya maisha yako. Ndoto bila mkakati maalum wa kufika itabaki kuwa ndoto kweli. Unahitaji kuwa na malengo yaliyoandikwa. Malengo ya muda mrefu na muda mfupi. Kila siku unakuwa unasukuma agenda kuelekea malengo ya muda mrefu... Malengo ni mwongozo sahihi kuishi kusudi lako na kufikia unakotaka kwenda. 3. Kuwa na mpango kazi wa kila siku. My friend, never start a day without having a plan. Ukumbuke, siku moja moja inakuwa inaongeza thamani kwenye malengo yako. Sio unaamka tu kuishia kwenye mishe. Hapana. Kila siku jiwekee utaratibu wa kupanga nini ufanye na kwa wakati gani. Ukitaka kuwa consistent, hii tabia itakusaidia sana. 4. Ukiweka malengo waambie watu ili ukomae kutowaangusha. Hii ni njia bora sana ya kubaki kwenye mwendelezo wa kila siku. Mf. Unataka kuacha kula sukari. Unawaambia marafiki wa karibu. Kila siku unakomaa kuhakikisha wanaona umeacha sukari... Baada ya muda kidogo unasahu kama wanakufatilia na kuwa tabia yako. Hii ni njia bora sana ya kuhakikisha hauishii njiani na kuwa na mwendelezo kukamilisha kile unafanya. 5. Jiheshimu. Kama vile unavyopewa assignment shule na kuifanya. Kama vile unavyopewa kazi na boss wako na kuifanya. Ndivyo hivyo unahitaji kufanyia kazi ndoto na malengo yako kama umetumwa na mtu unaemuheshimu. Ndo maana nakazia. JIHESHUMU... Watu wengi wanapenda kutii wengine, lakini wakijiwekea malengo yao hawayafati.

0 Comments

banner

Ahsante kwa kutembelea zotekali blog ili kuwa karibu nasi kila wakati Jiunge katika kurasa zetu zamitandao ya kijamii  facebook , Twitter, Instagram na Youtube  NI BUREE