Fahamu sababu za kuweka 'Flight Mode' unapokuwa kwenye ndege

"Tafadhali hakikisha viti vyako viko wima, toa kitambaa cha macho, kompyuta mpakato na vifaa vya elektroniki viwe katika hali ya 'airplane mode."


Ni wazi vitu hivi vinasababu zake? Vitambaa vya kuziba macho vinapaswa kuondolewa ili tuweze kuona ikiwa kuna dharura, kama moto.


Meza zinazoweza kurudishwa lazima zikunjwe na viti viwe wima ili tuweze kutoka nje ya kiti haraka iwezekanavyo.


Kompyuta za mpakato zinaweza kuwa silaha wakati wa dharura, kwa kuwa mifuko kwenye migongo ya viti haina nguvu ya kutosha kuzizuia.


Kuhusu simu janja , lazima ziwe katika hali 'airplane mode' ili zisiweze kuathiri vifaa vya ndani ya ndege. Teknolojia imetoka mbali sana


Uelekezaji wa ndege na mawasiliano yake yanatokana na mifumo ya redio, ambayo tangu miaka ya 1920 imeboreshwa ili kupunguza mwingiliano.


Kuhusu teknolojia ya digitali ambayo inatumika leo, ni ya juu zaidi kuliko teknolojia ya zamani ya analogia ambayo ilitumika hadi miaka 60 iliyopita.


Utafiti umeonyesha kuwa vifaa binafsi vya kielektroniki vinaweza kutoa mawimbi ndani ya bendi ya masafa sawa na mifumo ya mawasiliano ya ndege na uongozaji, na hivyo kuunda kinachojulikana kama kuingiliwa kwa sumakuumeme. Snake


Uingiliaji wa nchi kavu husababisha marufuku ya matumizi ya simu janja bila 'airplane mode'.


Lakini mwaka 1992, Mamlaka ya Usafiri wa Anga ya Merekani na Boeing, katika uchunguzi huru, walichunguza ikiwa utumiaji wa vifaa vya elektroniki ulisababisha usumbufu kwenye ndege na hakuna tatizo kwa kompyuta au vifaa vingine vya elektroniki vya binafsi wakati havifanyi kazi pamoja. wakati muhimu wa ndege (kuondoka na kutua huchukuliwa kuwa awamu muhimu).


Tume ya Mawasiliano ya Shirikisho la Marekani iliamua kuunda masafa tofauti kwa matumizi tofauti ya simu janja, uongozaji na mawasiliano ya ndege ili yasiingiliane. Serikali kote ulimwenguni zilitengeneza mikakati na sera sawa za kuzuia kuingiliwa.


Katika Umoja wa Ulaya, vifaa vya kielektroniki vilivyowashwa vimeruhusiwa tangu 2014.


Kwa hivyo, kwa kanuni hizi za kimataifa, kwa nini sekta ya anga imeendelea kupiga marufuku matumizi ya simu za mkononi? Moja ya matatizo yapo katika kitu ambacho hakiwezi kutarajiwa: kuingiliwa duniani. Snake


Waendeshaji wa viwanja vya ndege nchini Australia na Marekani wameibua wasiwasi kuhusu usalama wa anga kuhusiana na utolewaji wa 5G.


Internet isiyotumia waya imeunganishwa safu ya minara kadhaa ambayo inaweza kuzidiwa kupita kiasi ikiwa abiria wanaosafiri kwa ndege watatumia simu zao kwa wakati mmoja. Idadi ya abiria waliosafiri kwa ndege mnamo 2021 ilikuwa zaidi ya bilioni 2.2 (nusu ya idadi ya abiria mnamo 2019).


Kwa upande mwingine, katika miaka ya hivi karibuni kiwango kipya cha mawasiliano ya wireless kimepitishwa. Mitandao ya sasa ya 5G inayohitajika kasi ya juu ya uhamishaji data imesababisha wasiwasi katika sekta ya usafiri wa anga.


Kipimo cha data (bandwidth) ya masafa ya redio ni kidogo, hata hivyo, majaribio bado yanafanywa ili kuongeza vifaa zaidi. Sekta ya usafiri wa anga inabainisha kuwa wigo wa kipimo data cha mtandao usiotumia waya wa 5G uko karibu sana na wigo wa kipimo cha data uliotengwa kwa ajili ya usafiri wa anga, ambayo inaweza kusababisha kuingiliwa na mifumo ya uongozaji ndege inayosaidia ndege kutua.


Waendeshaji wa viwanja vya ndege nchini Australia na Marekani wameibua wasiwasi kuhusu usalama wa usafiri wa anga kuhusiana na utolewaji wa 5G, ingawa inaonekana kuwa Umoja wa Ulaya umefanya kazi vizuri.


Kwa vyovyote vile, inaonekana ni jambo la busara kupunguza matumizi ya simu za mkononi kwenye ndege huku masuala yanayohusiana na 5G yakitatuliwa. Hatimaye, hatuwezi kusahau usumbufu


Leo, mashirika mengi ya ndege hutoa huduma za Wi-Fi bila malipo au za kulipia kwa wateja wao. Kwa teknolojia mpya za Wi-Fi, abiria wanaweza, kwa nadharia, kutumia simu zao za mkononi kupiga simu za video na marafiki au wateja wakati wa safari ya ndege


Kuna wafanyakazi wa anga ambao wanaamini kuwa, abiria kuzungumza na simu wakiwa kwenye ndege inaweza kuwa usumbufu kwa maendeleo ya kazi zao.


Katika safari ya hivi karibuni, mhudumu wa ndege na aliulizwa maoni yake kuhusu kutumia simu wakati wa safari za ndege. Alisema kuwa itakuwa vigumu kwa wafanyakazi wa ndege kusubiri abiria kumaliza simu zao ili kuuliza kama wangependa vinywaji au chakula chochote.


Kwenye ndege iliyo na zaidi ya abiria 200, huduma ya ndani ingechukua muda mrefu kukamilika ikiwa kila mtu yuko kwenye simu.


Kwangu mimi, suala la matumizi ya simu ndani ya ndege linahusiana zaidi na hali ya kijamii ya kuwa na watu zaidi ya 200 kwenye ndege kuzungumza mara moja.


Katika umri ambapo tabia kuvurugana za abiria, ikiwa ni pamoja na uhasama, inazidi kuenea, matumizi ya simu ndani ya ndege yanaweza kuwa kichochezi kingine ambacho hubadilisha kabisa hali ya usafiri wa anga.


Tabia ya usumbufu hutokea kwa njia nyingi, kuanzia kushindwa kutii mahitaji ya usalama, kama vile kutovaa mkanda, mabishano ya matusi na abiria wengine na wafanyakazi wa ndani, hadi mabishano ya kimwili na abiria na wafanyakazi, ambayo kwa kawaida hutambuliwa kama hasira ya anga.


Kwa kumalizia, matumizi ya simu wakati wa safari ya ndege haiathiri kwa sasa uendeshaji wa ndege. Lakini wafanyakazi wa ndege hawapendi kuchelewa kutoa huduma za ndani ya ndege kwa abiria wote: kuna watu wengi wa kuwahudumia.


Hata hivyo, teknolojia ya 5G inaathiri kipimo data cha redio cha mifumo ya uongozaji ndege; tunahitaji utafiti zaidi ili kuelewa jinsi 5G inavyoingilia uongozaji wa ndege wakati wa kutua. Tukumbuke kwamba tunapozungumza kuhusu awamu mbili muhimu zaidi (kupaa na kutua) za ndege, kuondoka ni hiari, lakini kutua ni lazima.

0 Comments

banner

Ahsante kwa kutembelea zotekali blog ili kuwa karibu nasi kila wakati Jiunge katika kurasa zetu zamitandao ya kijamii  facebook , Twitter, Instagram na Youtube  NI BUREE